Showing posts with label Kingamwili.Corona.COVID19. Show all posts
Showing posts with label Kingamwili.Corona.COVID19. Show all posts

Tuesday, April 28, 2020

JE, UNAIFAHAMU KINGA DHIDI YA COVID19?

Kinga Madhubuti Dhidi Ya COVID19


  • Mwili unapoambukizwa na virusi🦠🦠vya COVID19, mfumo wake wa kinga (Immunity System)huanza kutengeneza kingamwili (antibodies)ambazo huwa na uwezo wa kutambua na kupambana na virusi ðŸ¦ ðŸ¦ ðŸ¦ na hatimae kinga ya mwili ikiwa imara virusi ðŸ¦ ðŸ¦ hivi kuondolewa mwilini kabisa. 
  • Mtu akipona maana yake ameweza kutengeneza kingamwili (Antibodies)za kutosha zilizofanikiwa kuondoa virusi ðŸ¦ ðŸ¦ vyote.
  • Licha hivyo kinga ya mwili (immunity system)pia hutengeneza seli za kumbukumbu(memory cells) kwa ajili ya kuukumbusha mwili endapo maambukizi yatajitokeza kwa mara nyingine.
  • Hivyo basi kuna uwezekano wa kuchukua Utegili (plasma)kutoka kwenye damu ya watu waliopona ambayo huwa na kingamwili(antibodies) dhidi ya virusi🦠🦠vya COVID19kuwapatia  wagonjwa mahututi wa Corona ili kusaidia wapate kinga itakayosaidia kuviondoa virusi🦠🦠ndani ya miili yao.
  • Kitendo hiki pia kinaweza kufanywa kwa watu wasio na maambukizi ya COVID19 ili kuwezesha wili kutengeneza kinga ya pili (secondary immunity)
  • Tiba hii inaitwa Convalescent Plasma Therapy, ni tiba ya muda mrefu na matabibu wameitumia kwa muda mrefu.