Tuesday, April 28, 2020

JE, UNAIFAHAMU KINGA DHIDI YA COVID19?

Kinga Madhubuti Dhidi Ya COVID19


  • Mwili unapoambukizwa na virusi🦠🦠vya COVID19, mfumo wake wa kinga (Immunity System)huanza kutengeneza kingamwili (antibodies)ambazo huwa na uwezo wa kutambua na kupambana na virusi ðŸ¦ ðŸ¦ ðŸ¦ na hatimae kinga ya mwili ikiwa imara virusi ðŸ¦ ðŸ¦ hivi kuondolewa mwilini kabisa. 
  • Mtu akipona maana yake ameweza kutengeneza kingamwili (Antibodies)za kutosha zilizofanikiwa kuondoa virusi ðŸ¦ ðŸ¦ vyote.
  • Licha hivyo kinga ya mwili (immunity system)pia hutengeneza seli za kumbukumbu(memory cells) kwa ajili ya kuukumbusha mwili endapo maambukizi yatajitokeza kwa mara nyingine.
  • Hivyo basi kuna uwezekano wa kuchukua Utegili (plasma)kutoka kwenye damu ya watu waliopona ambayo huwa na kingamwili(antibodies) dhidi ya virusi🦠🦠vya COVID19kuwapatia  wagonjwa mahututi wa Corona ili kusaidia wapate kinga itakayosaidia kuviondoa virusi🦠🦠ndani ya miili yao.
  • Kitendo hiki pia kinaweza kufanywa kwa watu wasio na maambukizi ya COVID19 ili kuwezesha wili kutengeneza kinga ya pili (secondary immunity)
  • Tiba hii inaitwa Convalescent Plasma Therapy, ni tiba ya muda mrefu na matabibu wameitumia kwa muda mrefu.